Saturday 3 January 2015

Shaaban Robert

Shaaban Robert ni mshairi, fasihi  na mwandishi mahiri ambaye anamchango mkubwa katika kuendeleza tamaduni na lugha adhimu ya kiswahili, Shaaban Reobert ni fahari ya Tanzania.

MAISHA YAKE:

Shaaban Robert alizaliwa Januari mosi, 1909 Kijiji cha Vibambani, jirani na Machui, kilomita 10 kusini mwa mji wa Tanga, alipata elimu yake katika Shule ya Msimbazi, jijini Dar es Salaam kati ya mwaka 1922 na 1926, alifaulu na kupata cheti.

Alikuwa mshairi na mwandishi wa riwaya. Mchango wake katika lugha ya Kiswahili ni mkubwa, kwani kazi zake zinaheshimika katika fasihi ya Kiswahili na zinatumika mashuleni. Alifariki dunia Juni 22, 1962.

Aliajiriwa na serikali ya kikoloni akawa karani katika Idara ya Forodha huko Pangani mwaka 1926 – 1944. Bila shaka kukaa kwake miaka mingi hivi katika mji wa kihistoria uliokuwa mahali pa utamaduni wa Kiswahili tena mahali patulivu, kumesaidia maendeleo yake Shaaban kama mwandishi wa Kiswahili.
Tangu mwaka 1944 alihamia ofisi nyingine ya Hifadhi ya Wanyama, baadaye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Mbali na maandiko yake, alikuwa na athari kubwa katika maendeleo ya lugha ya Kiswahili akiwa mjumbe wa kamati za East Africa Swahili Committee, East Africa Literature Bureau na Tanganyika Languages Board.

Kwa ujumla Shaaban Robert aliandika vitabu ishirini na viwili. Baadhi ya vitabu hivi ni Adili na Nduguze, Kusadikika, Kufikirika, Wasifu wa Siti Binti Saad, Baada ya Miaka Hamsini, na Maisha Yangu. Vitabu vyake vimetafsiriwa katika lugha za Kichina, Kiingereza na Kirusi. Alifariki dunia Juni 22, 1962 na kuzikwa Machui. Aliacha wake watatu na watoto kumi.

Kazi alizofanya alipokuwa karani wa serikali:
Akiwa serikalini alifanya kazi forodhani Pangani na mahali pengine tangu mwaka 1926 hadi 1944; Idara ya Wanyama tangu mwaka 1944 hadi 1946; na Ofisi ya Mkuu wa Jimbo la Tanga tangu mwaka 1946 hadi 1952.

Sehemu zingine ni Ofisi ya Kupima Nchi Tanga, tangu mwaka 1952 hadi 1960.

Alipandishwa cheo kuwa Grade III Higher Division mwaka 1929, na mwaka 1944 alipandishwa tena kuwa Grade II Local Service. Alikuwa mwanachama wa East African Swahili Committee, East African Literature Bureau, Tanganyika Languages, Tanga Township Authority.

Baadhi ya mashairi ya Shaaban Robert:

Kazi bora Afrika, yenye cheo na heshima.
Yapaswa kukumbuka, kuni ukulima.

Vibaya kuzohalika,kushika jembe kulima.
watu wengi wa asili, walikuwa wakulima.

Ubora wa jambo hili, yapaswa kuutazama.
Isipotee asili, makabila yakazama.

Ukulima ni halali, siyo kazi ya lawama.

Shaaban Robert pia alikuwa ni mtetezi wa heshima na haki za wanawake:

Si wajibu kusema, mke hana fadhili.
Wapo waume si wema, tia katika akili.

Na mabaya yanauma, hapana wa kuhimili.
Ukivunja heshima, mke naye hunakili.

ningojeni kina mama, mimi nitawatetea.
Tawatetea lawama, la ovyo lisilo njia

Litaondoka lazima,kwa upesi kukimbia
Mwisho mtajaliwa, nanyi mpewe heshima.

Shaaban Robert pia alikuwa ni mwalimu wa Tabia na maadili mema:

Ambapo anatuambia kuwa thamani ya mtu ni maadili mema si utajiri, nguvu wala ufahari;

Wapo watu maskini, hawana cha kutumia
Lakini wana thamani,kwa ubora wa tabia
Watu hao duniani, ni chumvi ya kutumia
Utatukuka jina, kwa uzuri wa tabia.

Wapo wenye milki, watakavyo hutumia
Lakini si marafiki, kwa ubaya wa tabia
Hao hawachukuliki,hatari kukaribia
Utatukuka jina, kwa uzuri wa tabia.

KIFO CHAKE

Marehemu Shaaban Robert alifariki Tanga Juni 22, 1962, alizikwa Machui, Tanga. Alituzwa zawadi ya waandishi inayojulikana kama ‘Margaret Wrong Memorial Prize’na nishani ya M.B.E.

Mungu ilaze roho ya Shaaban Robert mahala pema peponi.

Thursday 6 November 2014

BANJO SHORT FILM


This began as an idea for a pilot TV series, it was put together by a team of 8 people most of whom were ex students of St Johns Film department Cork. We choose to put the film online to build an audience and now plan to enter film festivals which accept films already online. Watch the film, let us know what you think and share the link The story
Code named BANJO, illegal immigrant JUMA PANJA(selector slim ) finds himself in the grip of notorious Irish crime boss MR. GOODMAN. When Banjo’s first job for his new boss goes wrong, he sets about trying to retrieve the lost loot with MR. GOODMAN’S short tempered and heavily tattooed bodyguard PADDY. 
Things take a turn for the worse when they stumble upon a lunatic farmer wearing flowery Wellington boots and his conniving son and stoner MIKEY. 
When BANJO and PADDY get kidnapped by the father and son team, BANJO is convinced it is the end for him and his new partner in crime, but after the farmer makes racial references to BANJO, PADDY makes the decision that it is do or die time, and so begins an hilarious three way standoff in a remote corn field in southern Ireland, but when the dust settles and they can’t find the money, there’s still one thing left to do. 
Break the news to MR. GOODMAN.

Tuesday 12 August 2014

Robin Williams Afariki Dunia, Dhana Kuwa Amejiua


Mwigizaji na mchekeshaji maarufu na mshindi wa nishani ya mwigizaji bora (Oscar-winning actor), amefariki dunia siku ya Jumatatu, 11th Agosti 2014. Habari zilizoko kwenye vyombo vya habari ni kwamba, Robin Williams amejiiua akiwa nyumbani kwake uko Kaskazini mwa California akiwa na umri wa miaka 63. Msemaje wake Buxbaum aliwaambia waandishi wa habari katika taarifa kuwa... Hivi karibuni Williams alikuwa anaosumbuliwa na unyogovu wa akili (depression), tatizo ambalo limesababishwa na matatizo ya unywaji mkubwa wa pombe. Ni tatizo ambalo limekuwa likimsumbuwa muda mrefu wa maisha yake.

Baadhi ya filamu alizo igiza ni kama hizi:

The World According to Garp (1982), Good Morning, Vietnam (1987), Dead Poets Society (1989), Awakenings (1990), The Fisher King (1991), and Good Will Hunting (1997), Popeye (1980), Hook (1991), Aladdin (1992), Mrs. Doubtfire (1993), Jumanji (1995), The Birdcage (1996), Night at the Museum (2006), and Happy Feet (2006), Everyone's Hero (2006), RV (2006), The Night Listener (2006), License to Wed (2007), August Rush (2007), Shrink (2009), World's Greatest Dad (2009), Night at the Museum: Battle of the Smithsonian (2009), Old Dogs (2009), Happy Feet Two (2011), Stage Left: A Story of Theater in the Bay Area (2011), The Big Wedding (2013), The Face of Love (2013), The Butler (2013), Boulevard (2014), The Angriest Man in Brooklyn (2014), Merry Friggin' Christmas (2014), Night at the Museum: Secret of the Tomb (2014).

Sunday 10 August 2014

MASHABIKI WA MR BACHCHAN

Mie ni mpenzi mzuri wa movie za kizungu  na kihindi na pia huwa nafuatilia Sana maisha yao. 
Naomba sana siku moja hii iwe inawatokea WASANII wa nyumbani.

Hiki ndio alichoandika mr mwenyewe
Na hii ni picha yake au post yake ya 674 ktk mtandao wa face book

FB 674-Sunday well wishers back again even after 32 years they still come...!!so humbled and filled with gratitude! Iwas away for a few Sundays but they still come so this evening it was a reunion...

Amitabh Bachchan



Mashabiki wakiwa nje ya nyumba ya mr Bachchan 
Yaani hawa wanaenda pale kumuona tu

Sunday 27 July 2014

Eid Mubarak

Assalamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh


Jumatatu In-shaa-Allah ni tarehe 1 Shawwaal 1435H (28 July 2014) na ndio Siku kuu yetu ya ‘Iydul-Fitwr.

Kwa Munaasabah huu wa furaha ya siku hii tukufu ya ‘Iyd Al-Fitwr Napenda kuchukua fursa hii kuwawasilishia salaam zetu mimi na Familia yangu za siku hii na du'aa njema kwenu wote, tukimuomba Allah (Subhaanahu Wa Ta'ala) Atutaqabalie 'amali zetu na zenu.